Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua ziada zinahitajika Sudan Kusini kudhibiti uhaba wa chakula, anasema Ofisa wa UM

Hatua ziada zinahitajika Sudan Kusini kudhibiti uhaba wa chakula, anasema Ofisa wa UM

Hilde F. Johnson, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) ametoa mwito unaopendekeza kuchukuliwe hatua ziada Sudan Kusini, ili kudhibiti tatizo la upungufu mkubwa wa chakula, uliojiri kwa sasa, katika baadhi ya sehemu za eneo, ili hali isije ikageuka kuwa janga baya zaidi.