Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO yahimiza ugawaji wa mapema wa dawa kinga dhidi ya H1N1

WHO yahimiza ugawaji wa mapema wa dawa kinga dhidi ya H1N1

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza hadhari maalumu kwa madaktari, inayowasihi kutongojea matokeo ya vipimo vya maabara ya afya kuhusu maambukizi, kabla ya kugawa dawa ya kupambana na virusi vya homa ya mafua ya A/H1N1 kwa wanawake wajawazito wanaodhaniwa wameambukizwa na maradhi hayo.