Sheria kali lazima zitekelezwe kuhifadhi mali ya asili kwenye mazingira ya mapigano, inasema ripoti ya UNEP
Shirika la UM juu ya Hifadhi ya mazingira (UNEP) limechapisha ripoti mpya, ilioandaliwa na wataalamu wa sheria, inayozingatia kanuni zinazohitajika kubuniwa na kuimarishwa ili kutunza mazingira, wakati wa mapigano, uhasama, vurugu na vita.