Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM azisihi serikali za kimataifa kuzingatia kikamilifu matatizo ya uhamaji

KM azisihi serikali za kimataifa kuzingatia kikamilifu matatizo ya uhamaji

Mnamo siku ya leo, KM Ban Ki-moon ambaye yupo Athens, Ugiriki akihudhuria Mkutano Mkuu wa Tatu wa Dunia juu ya Fungamano kati ya Maendeleo na Tatizo la Uhamaji, alihadharisha kwenye hotuba yake kwamba sera zinazohusu kuruhusu wahamaji wa kigeni kuingia nchini au la, ni lazima zibuniwe kwa kutia maanani zile taarifa zenye uhakika na sio chuki na ubaguzi dhidi ya wageni.