Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ndege za WFP zimeanzisha operesheni za kudondosha chakula Sudan Kusini baada ya mvua kali kuharibu barabara

Ndege za WFP zimeanzisha operesheni za kudondosha chakula Sudan Kusini baada ya mvua kali kuharibu barabara

Shirika la UM Juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeanzisha, Alkhamisi iliopita, operesheni za kudondosha, kutoka angani, misaada ya chakula inayohitajika kuhudumia watu 155,600 katika Sudan Kusini, ambapo barabara hiko zimeharibiwa na mvua kali zilizonyesha katika siku za karibuni, na kukwamisha shughuli za kusafirisha misaada ya kihali kwenye eneo.