4 Novemba 2009
Kadhalika, Ijumanne, KM Ban Ki-moon alihutubia mkusanyiko wa viongozi wa kidini na wale wasiohusiana na dini, katika Kasri ya Windsor, juu ya ulazima wa kushughulikia kipamoja matatizo yanayoletwa na mabadiliko ya hali ya hewa ulimwenguni.