23 Oktoba 2009
John Holmes, Naibu KM juu ya Misaada ya Kiutu na Masuala ya Kufarajia Misaada ya Dharura, alipozuru jimbo la Karamoja, Uganda kaskazini Ijumaa ya leo, alisihi juu ya umuhimu wa kupunguza hatari ya maafa kwa kudhibiti bora athari za mabadiliko ya hali ya hewa kwenye sehemu hizo za nchi.