Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Huduma za ndege za UM, za kugawa misaada ya kiutu Ethiopia, zahatarishwa kusitishwa

Huduma za ndege za UM, za kugawa misaada ya kiutu Ethiopia, zahatarishwa kusitishwa

Jumuiya ya Kundi Linalotumia Huduma za Usafiri wa Ndege za Kugawa Misaada ya Kiutu, ambalo hujulikana kama Kundi la UNHAS, imetangaza leo kwamba italazimika kusitisha operesheni zake nchini Ethiopia - hasa kwenye lile Jimbo la raia Wasomali - kwa sababu ya upungufu wa fedha kutoka wahisani wa kimataifa.