Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya chakula Kenya ni ya wasiwasi kwa sababu ya ukame, kuhadharisha UM

Hali ya chakula Kenya ni ya wasiwasi kwa sababu ya ukame, kuhadharisha UM

Ripoti iliotolewa na Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) kuhusu chakula katika Kenya imeeleza kuwepo hali ya wasiwasi ya chakula nchini humo, inayoendelea kuathiri mamilioni ya raia wa Kenya, kwa sababu ya kutanda kwa ukame wa muda mrefu kwenye eneo la Pembe ya Afrika.