Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku Kuu ya Kuwahishimu Walimu Duniani

Siku Kuu ya Kuwahishimu Walimu Duniani

Tarehe ya leo, tarehe 05 Oktoba, huadhimishwa na UM kuwa ni ‘Siku ya Walimu Duniani\'. Kwa mujibu wa taarifa ya Kitengo cha Taasisi ya Takwimu ya Shirika la UM juu ya Ilimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), kuanzia 2007 hadi 2015 kulihitajika kuajiriwa walimu milioni 10.3 kwa walimwengu kuweza kukamilisha, kwa wakati, lengo la kuwapatia ilimu ya msingi watoto wote wa kiume na wa kike wanaostahiki kuhudumiwa kadhia hiyo.