Kampeni ya kupandisha miti bilioni duniani ilifanikiwa kupita kiasi, imeripoti UNEP
Imetangazwa hii leo kwamba ile kampeni ya kimataifa ya kuotesha miti bilioni moja katika ulimwengu, kwa madhumuni ya kujikinga na taathira za mabadiliko ya hali ya hewa, imefanikiwa kufikia kiwango kilichokiuka matarajio ya waandalizi wa mradi huo.