Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano Mkuu juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa

Mkutano Mkuu juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa

Kwenye Mkutano wa UM juu ya Taathira za Mabadiliko ya Hali ya Hewa, unaofanyika hapa Makao Makuu, KM Ban Ki-moon aliwahimiza wakuu wa Taifa na serikali 100, waliohudhuria kikao hicho kuharakisha, kwa vitendo, zile hatua za kudhibiti bora tatizo la kuongezeka kwa hali ya joto ulimwenguni ili kuihifadhi sayari yetu kwa vizazi vijavyo.