Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Angelina Jolie ashtushwa na hali ngumu kwenye kambi ya wahamiaji wa Usomali mipakani Kenya

Angelina Jolie ashtushwa na hali ngumu kwenye kambi ya wahamiaji wa Usomali mipakani Kenya

Angelina Jolie, msanii maarufu wa michezo ya sinema na Balozi Mfadhili wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) alifanya ziara ya siku moja, mnamo mwisho wa wiki iliopita, katika kambi ya wahamiaji ya Dadaab, iliopo kwenye mpaka kati ya Kenya na Usomali.