Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kikao cha 53 cha IAEA chafunguliwa rasmi Vienna

Kikao cha 53 cha IAEA chafunguliwa rasmi Vienna

Kikao cha 53 cha Baraza Kuu la la Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) kimeanza rasmi Ijumatatu mjini Vienna, Austria na kwenye risala ya ufunguzi KM alitilia mkazo ulazima wa kuwa na mfumo unaoridhisha utakaohakikisha udhibiti bora wa silaha za kinyuklia, na kuhakikisha hazitoenezwa kimataifa.