Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

NKM atoa mwito wa utendaji dhidi ya udhalilishaji wa wanawake

NKM atoa mwito wa utendaji dhidi ya udhalilishaji wa wanawake

Kwenye mkutano wa mawaziri kuzingatia masuala ya udhalilishaji na matumizi ya nguvu dhidi ya wanawake, unaofanyika kwenye mji wa Roma, Utaliana, hii leo, NKM Asha-Rose Migiro aliwaambia wajumbe wa kimataifa waliohudhuria kikao hicho ya kuwa madhila ya kutumia mabavu dhidi ya wanawake yaliongezeka zaidi mnamo mwaka uliopita, kwa sababu ya kuporomoka kwa shughuli za soko la fedha la kimataifa.