Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICBL yawahimiza wanachama wa UA kusafisha mabomu yaliotegwa Afrika

ICBL yawahimiza wanachama wa UA kusafisha mabomu yaliotegwa Afrika

Taasisi ya Kampeni ya Kimataifa Kupiga Marufuku Mabomu Yaliotegwa Ardhini (ICBL) imetoa taarifa maalumu kwenye mkutano wa kikanda, iliokuwa na makusudio ya kuwahamasisha wanachama wa Umoja wa Afrika (UA) kuongeza jitihadi zao kwenye huduma za kukomesha na kufyeka milele kutoka bara la Afrika, zile silaha za miripuko zilizotegwa ardhini, na pia kuhakikisha haki za wanusurika wa silaha hizo zinahishimiwa kikamilifu.