Taarifa juu ya hali ya maambukizi ya A/H1N1 katika dunia
Shirika la Afya Duniani (WHO) kwenye taarifa ya wiki kuhusu hali ya maambukizo ya homa ya mafua ya A/H1N1 llimeeleza ya kwamba katika nchi za kizio cha kusini ya dunia, ikijumlisha Chile, Argentina, New Zealand na Australia maambukizo ya maradhi yameshapita kilele na hivi sasa yameselelea kwenye kigezo wastani, wakati mataifa ya Afrika Kusini na Bolivia yanaendelea kukabiliwa na ongezeko la homa ya mafua.