Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nusu ya ardhi ya kilimo duniani ina funiko kubwa la miti, wanasayansi wathibitisha

Nusu ya ardhi ya kilimo duniani ina funiko kubwa la miti, wanasayansi wathibitisha

Matokeo ya uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Kilimo cha Misitu Duniani, uliotumia satelaiti, ulithibitisha kihakika kwamba karibu nusu ya ardhi yote iliolimwa duniani huwa imesitiriwa na funiko muhimu la miti, licha ya kuwa shughuli za kilimo, hasa katika nchi zinazoendelea ndio zinazodaiwa kusababisha uharibifu mkubwa wa misitu.