Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Miripuko mipya ya kipindupindu inaashiriwa Zimbabwe

Miripuko mipya ya kipindupindu inaashiriwa Zimbabwe

Peter Salama, Mkuu wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) katika Zimbabwe hii leo ametoa onyo lenye kuhadharisha kwamba ana hakika mripuko mpya wa maambukizo ya maradhi ya kipindupindu nchini upo njiani na hautoepukika, kwa sababu ya kuharibika kwa miundo mbinu ya nchi, hali ambayo ndio itakayochochea tatizo hilo la afya, kwa mara nyengine tena.