Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Huduma ndege za WFP katika Chad zafadhiliwa dola milioni moja

Huduma ndege za WFP katika Chad zafadhiliwa dola milioni moja

Imetangazawa kutoka Geneva ya kwamba Ndege za Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) zitafadhiliwa msaada wa dola milioni moja kutoka Serikali ya Marekani, utakaotumiwa kuhudumia misaada ya kiutu katika Chad kwa mwezi mmoja ziada. Mnamo siku za karibuni, WFP ilikabiliwa na tatizo la kusitisha huduma hizo kwa sababu ya upungufu wa fedha.