Walinzi amani wa Tanzania wawasili Darfur: UNAMID
Shirika la Vikosi vya Mchanganyiko vya UM-UA kwa Darfur (UNAMID) limetangaza kwamba wanajeshi walinzi amani 200 kutoka Tanzania leo wamewasili kujiunga na operesheni zake kwenye jimbo la magharibi la Sudan.