WFP inasema mapigano ya kikabila Sudan Kusini yakwamisha huduma za chakula kwa umma muhitaji
Msemaji wa Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) Ijumaa aliripoti kutoka Geneva ya kwamba mashambulio yaliotukia karibuni kwenye eneo la Akobo, Sudan kusini yatazusha tena vitendo vya fujo na mtafaruku, kwa sababu ya makundi yalionuia kulipa kisasi, hali ambayo inabashiriwa itasababisha vifo zaidi.