Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM ashtumu vikali mashambulio ya kikatili Sudan Kusini

KM ashtumu vikali mashambulio ya kikatili Sudan Kusini

Mashambulio yaliotukia Ijumapili katika Akobo, Jimbo la Jongeli, Sudan Kusini ambapo watu 161 wanaripotiwa waliuawa, ikijumlisha wanawake na watoto 100, wanaume watu wazime 50 na askari 11 wa kundi la SPLA yamelaaniwa vikali na KM hii leo, hali ambayo imemlazimisha kulielekeza Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani Sudan Kusini (UNMIS), kuchukua hatua za dharura kuhudumia wale wote waliodhurika na vitendo katili hivyo, na vile vile kushirikiana na wenye madaraka kurudisha amani haraka iwezekanavyo kwenye jimbo hili la mtafaruku.