Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afrika yaongoza mataifa katika kunyonyesha watoto wachanga: WHO

Afrika yaongoza mataifa katika kunyonyesha watoto wachanga: WHO

Shirika la Afya Duniani (WHO) lemeripoti kwamba bara la Afrika ni miongoni mwa maeneo machache ulimwenguni yenye kuongoza kwenye huduma za kunyonyesha watoto wachanga, licha ya kuwa eneo hili linakabiliwa na matatizo aina kwa aina ya kiafya na kiuchumi. WHO imeeleza pindi kiwango cha kunyonyesha watoto katika Afrika kitaongezeka kwa asilimia 90, inakadiriwa watoto wachanga milioni 1.3 wataokoka vifo kila mwaka.