Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama lasailia hali ya usalama katika Chad/JAK

Baraza la Usalama lasailia hali ya usalama katika Chad/JAK

Baraza la Usalama asubuhi lilifanyisha kikao cha hadhara kusailia hali ya usalama katika Chad na Jamhuri ya Afrika ya Kati (JAK). Mjumbe Maalumu wa KM anayeshughulikia huduma za ulinzi amani wa mataifa haya mawili, Victor Angelo, alipowakilisha taarifa yake mbele ya Baraza alisema jumuiya ya kimataifa inawajibika kuharakisha kufanyika majadiliano ya kidiplomasiya ili kurudisha utulivu na amani ya eneo, kufuatilia mapigano yalioripuka karibuni baina ya Chad na Sudan.