Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maambukizi ya A/H1N1 ni ya wastani kwa sasa, inasema WHO

Maambukizi ya A/H1N1 ni ya wastani kwa sasa, inasema WHO

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeripoti leo hii kwamba maambukizi ya janga la homa ya mafua ya A/H1N1 kimataifa yanakadiriwa kuwa bado ni ya wastani, na wingi wa watu wanaouguwa maradhi haya kwa sasa, kwa bahati, hawashuhudii maumivu makali na hawahitajiki kulazwa hospitali.