Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu milioni 6.2 Ethiopia wanakabiliwa na hatari maututi ya utapiamlo, OCHA inahadharisha

Watu milioni 6.2 Ethiopia wanakabiliwa na hatari maututi ya utapiamlo, OCHA inahadharisha

Fidele Sarassoro, Mratibu wa Misaada ya Kiutu katika Ofisi ya UM juu ya Huduma za Dharura (OCHA) ametangaza kwamba taifa la Ethiopia linakabiliwa kwa sasa na tatizo la kuhudumia mamilioni ya raia misaada ya kihali, kwa sababu ya upungufu wa chakula, huduma za afya, lishe bora pamoja na maji safi na usafi wa mazingira, ikichanganyika pia na matatizo ya ukosefu wa makazi ya dharura, ajira na ukosefu wa shughuli za kilimo ambazo zinahitajika kuwasaidia raia kupata riziki.