Machafuko ya makazi bora Afrika Kusini yanaitia wasiwasi UN-HABITAT
Shirika la UM juu ya Makazi (UN-HABITAT) limeripoti kuingiwa na wasiwasi kuhusu maandamano ya machafuko yaliozuka majuzi kwenye vitongoji vya Afrika Kusini, ambapo mamia ya watu walidai wapatiwe makazi madhubuti ya nyumba, pamoja na kupatiwa huduma za maji safi ya kunywa, umeme na mazingira yalio safi.