Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

OCHA inasema waasi wa Uganda wanaendelea kutesa raia katika JKK

OCHA inasema waasi wa Uganda wanaendelea kutesa raia katika JKK

Tawi la Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) iliopo Nairobi, Kenya limetoa taarifa yenye kuthibitisha waasi wa Uganda wa kundi la LRA, waliojificha kwenye maeneo ya kaskazini-mashariki, katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) wanaendelea kuhujumu na kuteka nyara, pamoja na kuua raia wa katika eneo.