Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua za dharura kwenye sekta ya afya zinahitajika Usomali kunusuru maisha ya waathirika wa mapigano na vurugu

Hatua za dharura kwenye sekta ya afya zinahitajika Usomali kunusuru maisha ya waathirika wa mapigano na vurugu

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeeleza kwamba mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yalioshtadi nchini Usomali kwa sasa hivi, yamesawijisha na kudhoofisha sana huduma za afya pamoja na miundombinu ya kijamii, hususan kwenye maeneo ya Kati na Kusini mwa nchi.