Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNOMIG yakamilisha rasmi uhamisho Georgia kufuatia kura ya vito ya Urusi

UNOMIG yakamilisha rasmi uhamisho Georgia kufuatia kura ya vito ya Urusi

Shirika la Uangalizi wa Kusimamisha Mapigano katika Georgia (UNOMIG) limeripoti kukamilishwa, kwa leo hii, uhamisho wa waangalizi wote wa kimataifa kutoka nchini humo, kufuatia kura ya vito ya karibuni ya Urusi kwenye Baraza la Usalama, kura ambayo ilipinga rai ya UM kuongeza muda wa operesheni za kusimamia amani kwenye eneo hili.