Togo kusaidiwa na Global Fund kupambana na janga la VVU/UKIMWI
Taasisi ya Mfuko wa Kimataifa dhidi ya Ukimwi, Kifua Kikuu [TB] na Malaria (Global Fund) imetia sahihi na Togo, maafikiano ya kuipatia msaada wa dola milioni 20 ili kutumiwa mnamo miaka miwili ijayo kuhudumia juhudi za kitaifa kudhibiti maambukizi ya VVU na maradhi ya UKIMWI.