Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR ina wasiwasi juu ya madai wanamaji wa Utaliana waliwatendea kusio huruma wahamiaji wa Eritrea

UNHCR ina wasiwasi juu ya madai wanamaji wa Utaliana waliwatendea kusio huruma wahamiaji wa Eritrea

Ron Redmond, Msemaji wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) ameripoti leo hii, kutokea Geneva, ya kuwa watumishi wa UNHCR waliopo Libya, walifanikiwa kufanya mahojiano na watu 82 waliozuiliwa karibuni na manowari za Utaliana, kwenye eneo la bahari kuu liliopo maili za bahari 30 kutoka kisiwa cha Utaliana cha Lampedusa.