Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe Maalum wa KM kwa Usomali ana matumaini utulivu utarejeshwa nchini karibuni

Mjumbe Maalum wa KM kwa Usomali ana matumaini utulivu utarejeshwa nchini karibuni

Wiki iliopita Kamishna Mkuu wa UM juu ya Huduma za Wahamiaji, Antonio Guterres, alibainisha kwamba tangu mapigano kufumka katika mji wa Mogadishu, mnamo mwanzo wa mwezi Mei, baina ya vikosi vya Serikali na makundi ya upinzani yaliojumuisha majeshi ya mgambo ya Al-Shabab na Hizb-al-Islam, watu 200,000 inaripotiwa walilazimika kuhajiri makazi, kiwango cha uhamaji ambacho kilishuhudiwa kieneo mara ya mwisho katika mwaka 2007, pale vikosi vya Ethiopia vilipoingilia kati, kwa nguvu, mgogoro wa Usomali.