Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu milioni 2.3 wenye VVU wafaidika na msaada wa 'Global Fund' wa dawa ya kurefusha maisha

Watu milioni 2.3 wenye VVU wafaidika na msaada wa 'Global Fund' wa dawa ya kurefusha maisha

Taasisi ya Mfuko wa Kimataifa Dhidi ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria – inayoungwa mkono na UM – yaani Taasisi ya Global Fund, imetangaza leo watu milioni 2.3 walioambukizwa na virusi vya UKIMWI ulimwenguni walifanikiwa kupatiwa ile dawa ya kurefusha maisha ya ARV, kutokana na miradi inayosimamiwa na Taasisi ya Global Fund. Muongezeko huu unawakilisha asilimia 31 ya watu waliohudumiwa tiba hiyo, tukilinganisha na takwimu za mwaka jana.