Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha Mashitaka wa ICC aitaka korti ya rufaa iruhusu kukamatwa raisi wa Sudan

Mwendesha Mashitaka wa ICC aitaka korti ya rufaa iruhusu kukamatwa raisi wa Sudan

Luis Moreno-Ocampo, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) ameripotiwa kutangaza kwamba ana ushahidi ziada, utakaomwezesha ofisi yake kutoa hati ya kukamatwa kwa Raisi Omar Al-Bashir wa Sudan, kwa madai alihusika na mauaji ya halaiki nchini kwao.