Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ripoti ya UM inasema, mafanikio ya karibuni kufyeka njaa na umaskini yanahatarishwa na mizozo ya chakula na uchumi

Ripoti ya UM inasema, mafanikio ya karibuni kufyeka njaa na umaskini yanahatarishwa na mizozo ya chakula na uchumi

"Ripoti ya UM juu ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs)" kwa mwaka huu, ilowasilishwa rasmi Geneva hii leo na KM Ban Ki-moon, ilitahadharisha ya kuwa mzoroto/mdodoro wa uchumi uliojiri ulimwenguni sasa hivi, na vile vile bei ya juu ya chakula ilioselelea kimataifa katika 2008, ni matukio yaliojumuika kurudisha nyuma yale maendeleo yaliopatikana miaka 20 iliopita ya kupunguza umaskini katika dunia.