Tiba ya majaribio dhidi ya usubi imeanzishwa rasmi katika nchi tatu za Afrika, imeripoti WHO
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuanzisha majaribio ya tiba mpya dhidi ya maambukizi ya maradhi ya usubi, katika mataifa matatu ya Afrika - yakijumlisha Ghana, Liberia na JKK.