Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mfuko wa CERF kuifadhilia IOM msaada wa kuhudumia makazi ya muda wahamiaji wa Usomali

Mfuko wa CERF kuifadhilia IOM msaada wa kuhudumia makazi ya muda wahamiaji wa Usomali

Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limeripoti kuwa litapokea msaada wa dola milioni 2.6 kutoka Taasisi ya Mfuko wa UM juu ya Maafa ya Dharura au Mfuko wa CERF, fedha zitakazotumiwa kuwasaidia kupata makazi ya dharura wahamiaji 12,700 wa Usomali ambao wanabanana hivi sasa kwenye kambi za Kakuma, ziliopo Dadaab, kwenye jimbo la kaskazini-mashariki ya Kenya.