Wataalamu wa UM wamehadharisha wajumbe wa Kikao cha BK juu ya Mzozo wa Uchumi kutosahau kufungamanisha haki za binadamu kwenye maamuzi yao
Magdalena Sepúlveda na Cephas Lumina, Wataalamu Huru wawili wa UM wanaohusika na masuala ya haki za kibinadamu kwenye mazingira ya umaskini uliovuka mipaka na kuhusu athari haribifu za madeni, wametuma taarifa maalumu kwenye Mkutano wa Baraza Kuu juu ya Mizozo ya Uchumi na Kifedha, iliohimiza Mataifa Wanachama "kuchukua hatua za dharura, zitakazosaidia kuendeleza ufufuaji wa muda mrefu wa shughuli za kiuchumi na fedha, kwa kutunza haki za kimsingi kwa umma mamskini wenye kusumbuliwa zaidi na matatizo haya ya kiuchumi" kwa kupatiwa huduma za jamii.