Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR ina wasiwasi na kunyanyuka kihadhi kwa vyama baguzi vipingavyo wageni katika EU

UNHCR ina wasiwasi na kunyanyuka kihadhi kwa vyama baguzi vipingavyo wageni katika EU

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limetoa mwito maalumu wenye kuisihi Serikali ya Sweden kutumia wadhifa uliokabidhiwa nao sasa hivi, wa uraisi wa Umoja wa Ulaya (EU), kutilia mkazo umuhimu wa nchi wanachama kusimamia shughuli za mipaka yao, kwa kuzitekeleza kanuni za huruma za kuruhusu wahamaji wa kigeni kupata hifadhi, kama ilivyoidhinishwa na haki za kimsingi za kiutu.