Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO inasema mamilioni ya hekta za savana Afrika zipo tayari kuvuna natija kuu za kibiashara ya kilimo

FAO inasema mamilioni ya hekta za savana Afrika zipo tayari kuvuna natija kuu za kibiashara ya kilimo

Ijumatatu Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limetangaza kwamba sehemu kubwa ya ardhi ya savanna, iliotanda katika mataifa 25 barani Afrika, pindi itadhibitiwa na shughuli za kiuchumi kama inavyostahiki, itamudu kuzalisha bidhaa za chakula, kwa wingi kabisa, hali ambayo italiingiza eneo miongoni mwa maeneo yatakayoongoza biashara ya bidhaa za kilimo kwenye soko la kimataifa.