Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uadui dhidi ya watumikia misaada ya kiutu Usomali wahatarisha maisha ya watoto na wanawake, imehadharisha UNICEF

Uadui dhidi ya watumikia misaada ya kiutu Usomali wahatarisha maisha ya watoto na wanawake, imehadharisha UNICEF

Kaimu Mwakilishi wa Shirika la UNICEF kwa Usomali, Hannan Sulieman amenakiliwa akisema, kutokea Nairobi, kuwa "ameudhika sana" na kuongezeka kwa mawimbi mapya ya mashambulio, uchokozi na uadui uliotanda siku za karibuni, dhidi ya wafanyakazi wanaohudumia misaada ya kiutu katika Usomali.