Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Dunia Dhidi ya Ajira ya Watoto Wadogo

Siku ya Dunia Dhidi ya Ajira ya Watoto Wadogo

Kwenye kumbukumbu ya miaka 10 ya Siku ya Dunia dhidi ya Ajira ya Watoto wa Umri Mdogo, siku ambayo huadhimishwa tarehe ya leo kulitolewa mwito maalumu na Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF), likijumuika na mashirika wenzi wa kuhimiza jamii ya kimataifa kukabiliana na sababu za msingi zenye kuchochea umasikini na ufukara, hali ambayo inaaminika ndio yenye kuwalazimisha watoto wenye umri mdogo kutafuta ajira ya kumudu maisha.