Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano Usomali yazusha msururu was maafa, mamia ya majeruhi na uhamisho wa lazima

Mapigano Usomali yazusha msururu was maafa, mamia ya majeruhi na uhamisho wa lazima

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti mapigano makali yalioshtadi katika mji mkuu wa Mogadishu, Usomali mnamo miezi ya karibuni, yamewacha nyuma msururu wa uharibifu na maangamizi, majeruhi kadha wa kiraia na kusababisha mamia elfu ya watu kulazimika kuhama makazi na kuelekea maeneo tofauti ya nchi yenye hifadhi bora.