Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya huduma za kiutu yataka kuanzishwe miradi ya kuhifadhi raia na athari za mabadiliko ya hewa

Mashirika ya huduma za kiutu yataka kuanzishwe miradi ya kuhifadhi raia na athari za mabadiliko ya hewa

Mashirika 18 ya UM yenye kuhudumia misaada ya kiutu, yakichanganyika na mashirika wenzi mengineyo yalio wanachama wa ile Kamati ya Kudumu ya Jumuiya Zinazotegemeana (IASC), yamependekeza kujumuishwa kwenye mkataba utakaofuatia Mkataba wa Kyoto, yale masuala yanayohusu athari haribifu dhidi ya wanadamu, zinazoletwa na mabadiliko ya hali ya hewa.