Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO yatoa mwito wa kubuniwa mfumo imara dhidi ya njaa

FAO yatoa mwito wa kubuniwa mfumo imara dhidi ya njaa

Jacques Diouf, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) ametoa mwito maalumu, uitakayo jamii ya kimataifa kuimarisha mfumo wa utawala bora wa kukabiliana na matatizo ya njaa, kwa kuhakikisha akiba ya chakula katika ulimwengu itadhaminiwa kwa taratibu zitakoridhisha na kutimiza mahitaji ya chakula ya muda mrefu kwa umma wa kimataifa.