Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM imepeleka mkono wa taazia kwa kifo cha raisi wa zamani wa Sudan

UM imepeleka mkono wa taazia kwa kifo cha raisi wa zamani wa Sudan

Mjumbe Maalumu wa KM kwa Sudan, Ashraf Qazi, leo amepeleka mkono wa taazia kwa umma wa Sudan pamoja na aila ya aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo, Raisi Jaafer Nimeiri, baada ya magazeti kuripoti rasmi taarifa iliotolewa na Serikali Ijumamosi kuhusu kifo cha Raisi Nimeiry. Marehemu Nimeiry alikuwa na umri wa miaka 79 na aliugua kwa muda mrefu ugonjwa usiotambulika.