WFP yafungua ofisi mpya Usomali ya Kati
Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limefungua ofisi mpya katika eneo la Usomali ya Kati. Hatua hii muhimu iliochukuliwa na UM inatarajiwa kurahisisha shughuli za kuhudumia chakula watu muhitaji milioni moja ziada, waliokuwa wakitegemea shirika lisio la kiserikali, ambalo liliondoka nchini mwaka jana, kwa sababu ya ukosefu wa usalama wa wafanyakazi.