Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utabiri wa DESA juu ya hali ya uchumi duniani kwa 2009

Utabiri wa DESA juu ya hali ya uchumi duniani kwa 2009

Idara ya UM juu ya Masuala ya Kiuchumi na Jamii (DESA) asubuhi iliwasilisha rasmi, ripoti ya katikati ya mwaka, yenye mada isemayo “Hali ya Uchumi Duniani na Matumaini kwa 2009”. Ripoti ilibashiria uchumi wa ulimwengu kwa mwaka huu utateremka kwa asilimia 2.6, baada ya huduma za kiuchumi kupanuka kwa asilimia 2.1 katika 2008, na baada ya kupanuka, vile vile, kwa karibu asilimia 4 kila mwaka katika kipindi cha baina ya 2004 na 2007.